Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Yusuf Masauni amesema ataunda kamati ya wataalamu kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa magari yote ya polisi 119 yaliyopo bandarini na 53 ya Chuo cha Mafunzo cha Polisi Kurasini.
Mhandisi Masauni amefikia uamuzi huo baada ya kubaini magari matano kati ya 53 ya Chuo cha Mafunzo cha Polisi Kurasini yana hitilafu mbalimbali.
Naibu Waziri huyo, ameeleza hayo leo Jumanne, Januari 2, 2018 wakati alipofanya ziara ya kukagua magari hayo katika maeneo ya bandarini na katika chuo hicho.
Amesema kamati hiyo itajumuisha wataalamu mbalimbali kutoka na idara mbalimbali za Serikali ili kuja na majibu ya kina kuhusu hitilafu hizo.
Mhandisi Masauni amesema bandarini kuna magari ambayo ni malori, hivyo kamati hiyo itachunguza mikataba ya uagizaji wa magari hayo kwa kuwa ni aina moja wakati polisi inauhitaji wa aina mbalimbali za usafiri.